ZIARA YA MHESHIMIWA JAJI MKUU UNGUJA
HABARI
Mhe Jaji Mkuu wa Zanzibar
Mhe Khamis Ramadhan Abdalla amewataka wafanyakazi wa Mahkama kuwahudumikia Wananchi
wanaokuja Mahkamani kupata huduma kwa kutumia lugha nzuri na kuwafahamisha taratibu zote za kimahkama kwa uwazi kabisa bila ya upendeleo wowote
ule.
Hayo aliyasema kwenye ziara zake za kuzitembelea Mahkama za Unguja
ili kujionea utendaji kazi wa Mahkama
hizo na kusikiliza changamoto na kuzipatia ufumbuzi.
Aidha Mhe Jaji Mkuu amewaagiza
Mahakimu dhamana wa Vituo hivyo kutenga
siku Maalumu kwa Ajili ya kusikiliza Malalamiko kwa wananchi na kuyatafutia
ufumbuzi.
Kwa upande wake Mrajis wa
Mahkama Kuu Mhe Valentina A. Katema aliwapongeza wafanyakazi wa Mahkama hizo
kwa kazi nzuri wanazozifanya.
Aidha Mhe Mrajis aliwataka wafanyakazi wa
Mahkama kuhakikisha kuwa hati za wito wa
Mahkama zinatolewa Mapema ili kuwafikia
wahusika mapema.
Nao wafanyakazi wa
Mahkama hizo wakieleza changamoto zinazowakabili walisema wanakabiliwa na
uchache wa wafanyakazi kwenye vituo vyao vya kazi na ufinyu
wa nafasi katika Majengo ya Mahkama.
Kwa upande mwengine Mhe
Jaji Mkuu wa Zanzibar amekabidhi Magari Mapya kwa Majaji Watatu na Kadhi Mkuu akizigumza wakati wa
makabidhiano hayo Mhe Jaji Mkuu aliishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
kwa kuwapatia Magari hayo ili kuondoa changamoto ya Usafiri kwa watumishi wa
Mahkama.
Nae Mhe Kadhi Mkuu wa
Zanzibar kwa niaba ya wahesimiwa Majaji alishukuru kwa kupatiwa Magari hayo na
kuhakikisha kuwa watayatunza katika kipindi chote cha utumishi wao.