A PHP Error was encountered

Severity: Warning

Message: fopen(/var/cpanel/php/sessions/ea-php80/ci_session02262ec9bd4bd3ee8ff5a2e4c06d2bd73056c441): Failed to open stream: No space left on device

Filename: drivers/Session_files_driver.php

Line Number: 176

Backtrace:

File: /home/court/public_html/web/application/controllers/Posts.php
Line: 23
Function: __construct

File: /home/court/public_html/web/index.php
Line: 315
Function: require_once

A PHP Error was encountered

Severity: Warning

Message: session_start(): Failed to read session data: user (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php80)

Filename: Session/Session.php

Line Number: 143

Backtrace:

File: /home/court/public_html/web/application/controllers/Posts.php
Line: 23
Function: __construct

File: /home/court/public_html/web/index.php
Line: 315
Function: require_once

The Judiciary of Zanzibar

Registrar: registrar@judiciaryzanzibar.go.tz | Chief Court Administrator: cca@judiciaryzanzibar.go.tz

THE JUDICIARY OF ZANZIBAR

JAJI MKUU AFUNGUA MKUTANO WA KUMI NA 17 WA ZAJOA

Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Khamis Ramadhan Abdalla amewataka Majaji, Mahakimu na Makadhi kufanya kazi zao kwa uweledi na kujiamini  katika kutoa haki bila ya kuingiliwa katika utoaji wa maamuzi yao.

  Ameyasema hayo Leo katika Mkutano wa 17 wa Chama Cha Majaji na Mahakimu Zanzibar  uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi.

  Amesema Mahakama ni chombo huru ambacho kinafanya kazi zake bila ya kusimamiwa na taasisi nyengine yeyote.  Pia amewashauri Majaji na Mahakimu pamoja na Makadhi kujiamini na kuhakikisha wanatoa maamuzi ya mashauri kwa wakati ili kupunguza malalamiko ya wananchi kuhusu ucheleweshaji wa kesi.

     Aidha Jaji Mkuu ameishukuru serikali ya awamu ya nane inayoongozwa na Dkt Hussein Ali Mwinyi kwa kuwapatia vitendea kazi na kuwaomba wanachama hao kuvitunza na kutumia vitendea kazi katika kuandikia hukumu za mashauri  pamoja na kuhakikisha mienendo ya kesi inapatikana kwa wakati.

      Kwa upande wake Jaji wa Mahkama Kuu Mhe. Salma Ali Hassan ambae pia ni Raisi wa Chama hicho amesema kukutana kwao kwa pamoja ni fursa adhimu ambayo inapelekea kutatua changamoto zinazowakumba katika kazi zao za kila siku za utoaji hukumu kwa wananchi pamoja na kuelezea mafanikio yanayo patikana kutoka katika Jumuia hiyo.

      Jumuia  ya Majaji ,Mahakimu na Makadhi  (ZAJOA) imeanzishwa mwaka 2007 ambapo imewakutanisha  Majaji Mahakimu  na Makadhi wa Mahkama ya Zanzibar.

Unguja

High Court, Vuga
ZANZIBAR
Tel: +255 719 606 436
Email: info@judiciaryzanzibar.go.tz
Monday - Friday: 07:30am - 09:30pm
Saturday & Sunday: Closed

Pemba

High Court, Chake-Chake
ZANZIBAR
Tel: +255 719 606 436
Email: infopemba@judiciaryzanzibar.go.tz
Monday - Friday: 07:30am - 09:30pm
Saturday & Sunday: Closed